Na Shufaa Lyimo
Shirikisho la soka Tanzania TFF linatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa kujadili mambo mbali mbali ya soka mwanzoni mwa mwezi March mwaka huu.
Akizungumza na Championi hivi karibuni Rais wa Tff Leodgard Tenga alisema kuwa,lengo na dhumuni la kufanya mkutano huo ni kutaka kupanua soka zaidi hasa kwa vijana wadogo wanaochipukia sasa hivi.
Hata hivyo tutajadili mambo mbalimbali ya kuboresha soka Tanzania ikiwa ni pamoja na kutafuta njia za kufanya ili vilabu vyetu viwe na sifa mojawapo ya kuepukaka migogoro inayojitokeza mara kwa mara katika klabu zetu.
"Katika mkutano huo tutahakikisha tutakaalo lizungumza tutalifanyia kazi na kuboresha soka nchini Tanzania kama jinsi wenzetu wanavyofanya katika nchi zao kwa kuweka soka kuwa kipao mbele" Alisema Tenga.
Vile vile aliendelea kusema kwamba, sasa hivi Tanzania imepanuka sana kisoka na katika kikao hicho watafanya mambo ambayo yatawabadilisha viongozi mbali mbali wa Klabu na kuwaletea mafanikio makubwa.
Sunday, January 20, 2008
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment