Na Chausiku Omary.
Kumbe chama cha mpira wa mikono nchini (TAHA) mwenendo wake ni kama chama cha makocha wa soka nchini TAFCA kutokana na kuendesha elimu kwa makocha wao.
Akizungumza na Championi mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa chama hicho David Mataka, alisema kuwa mafunzo hayo yataendeshwa kwa muda wa wiki moja kwenye Kanda tano tofauti kwa kuwashirikisha waalimu na waamuzi wa mchezo huo.
"Kozi hizo zinalenga walimu na wa mchezo huu kutoka shule za msingi na vyuo tunahitaji ushirikiano wao zaidi ili kuweza kufanikisha mafunzo hayo" alisema Mataka.
Mataka alizitaja kanda zitakazoshiriki katika mafunzo hayo kuwa ni Kanda ya Mashariki, Kusini, Kati, Ziwa na Kaskazini.
Sunday, January 6, 2008
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment