Sunday, January 6, 2008

Duh! Simba kila kona!

Mwenyekiti wa Simba ya Jijini Dar es Salaam, Mwina Kaduguda a.k.a Simba wa Yuda.

Na Khamis Bwanga, Kilindi

Kama ulikuwa hujui jinsi mnyama Simba alivyo hatari na mwenye nguvu basi soma habari hii kwa makini ili kujua nini kitatokea kwa mwaka huu.

Akizungumza na Championi mwishoni mwa wiki iliyopita wilayani Kilindi mkoani Tanga, Makamu Mwenyekiti wa Simba Omar Gumbo, alisema kwamba wameazimia kufungua matawi katika kila tarafa na kata kwa nchi nzima ili kuongeza wanachama.

"Ili kujiimarisha tumeamua kufungua matawi nchi nzima lengo ni kuongeza wanachama, na kwamba katika safari yangu hii ya Wilaya ya Handeni nimefungua tawi jipya na sasa tunatarajia kunzunguka nchi nzima kwa ajili ya zoezi kama hilo," alisema Gumbo.

Mwenyekiti huyo wa Simba yupo katika ziara ya mikoa ya Kanda ya Kaskazini, Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara kwa ajili ya kuhamasisha zoezi la uandikishaji wa wanachama wapya zoezi ambalo litaendelea nchi nzima.

No comments: